Friday, February 6, 2009

MUME BWEGE - BUSHOKE














Nilikuwa na mpenzi wangu

Nani asiyemjua

Mtoto kaumbika

Utasema malaika

Miezi kadhaa ikasogea

Mtoto (wa) kwanza tukazaa

Mtoto katoka Mwarabu

Swali lilikosa jibu

Akasema we hujui

Mtoto kafata kwa babu

Nikagunaguna pale mzee nikauchuna


Mtoto (wa) pili tukazaa

Huyu wa sasa Mchina doh

Nikasema mama vipi

Mbona mi sielewi

Akasema we hujui

Huyu kafata kwa bibi


Aa wewe mama wee

Ingekuwa ungefanyeje


Mwenzenu nalala chini

Mke wangu kitandani

Nikilala kitandani

Kila mtu shuka lake

Mwenzenu nalala chini

Mke wangu kitandani

Nikilala kitandani

Basi ujue mzungu wa nne


Nikiuliza kwa nini

Anasema amenipa likizo eeh

Siyo kama napenda

Imenilazimu ooh

Siyo kama napenda

Ananilazimisha yoo


Mwenzenu naosha vyombo

Mwenzenu napiga deki

Mzee mzima napika

Jamani nafua nguo

Siyo kama napenda

Nalazimishwa mimi


Lo, hii sasa kali

Jana kaniambia anataka kwenda klabu na marafiki zake

Ila kaniambia mimi

Nilinde nyumba eti wezi wasije wakaiba

Eee Bize Man hii halali kweli

Oyaa Mbiye njoo unisaidie huku nyumbani mwenziyo naonewa

Chifu Rumanyika, unajifanya hujui

Ooo naonewa mimi

Aa wewe mama wee

Ingekuwa ungefanyeje


MSAMIATI


-jua - fahamu

umbika - naturally attractive

mzungu wa nne - opposite direction

likizo - mapumziko

lazimu - ni lazima

lazimisha - force to do something

osha - wash

vyombo - dishes

piga deki - kusafisha sakafu

fua nguo - wash clothes

linda - protect

wezi - wingi wa mwizi

iba - steal

halali - fair

onea - mistreat




No comments:

Post a Comment